Ajenda Uturuki

Turkish Airlines Kurejesha Safari za Damascus, Beirut na Amman Mei Mosi

Shirika hilo lasema usalama wa anga umeimarika baada ya kusitisha safari tangu Februari kutokana na tahadhari za kiusalama.

Newstimehub

Newstimehub

30 Aprili, 2026

745

Shirika la ndege la Uturuki, Turkish Airlines, limetangaza kuwa litarejesha rasmi safari zake kuelekea miji ya Damascus nchini Syria, Beirut nchini Lebanon na Amman nchini Jordan kuanzia Mei 1 mwaka huu.

Kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti yake rasmi, shirika hilo limesema uamuzi huo umefikiwa baada ya tathmini mpya ya hali ya usalama wa anga katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Safari hizo zilikuwa zimesitishwa tangu Februari 28 kufuatia hofu ya kiusalama iliyotokana na mvutano wa kikanda na hatari zilizokuwa zikihusishwa na safari za anga katika eneo hilo.

Hatua ya kurejeshwa kwa safari hizo inatazamwa kama ishara ya kuimarika kwa hali ya usalama na kurejea kwa taratibu za kawaida katika sekta ya usafiri wa anga kwa baadhi ya maeneo ya Mashariki ya Kati.

CHANZO: TRT Afrika