Mwanariadha wa Kenya wa mbio za marathon, Sabastian Sawe, ameandika historia mpya duniani baada ya kushinda mbio za London Marathon kwa muda wa saa 1:59:30, na kuwa mwanariadha wa kwanza kukamilisha kilomita 42 chini ya saa mbili katika mashindano rasmi.
Ushindi huo pia umeambatana na rekodi mpya ya dunia, ambapo Sawe ameipiku rekodi ya awali iliyowekwa mwaka 2023 kwa sekunde 65.
Mafanikio hayo yamemfanya Sawe kuwa gumzo duniani, huku akitajwa kama mmoja wa wanariadha bora zaidi wa kizazi chake baada ya kuandika historia isiyowahi kufikiwa katika marathon.
CHANZO: TRT Afrika














