Mahakama ya Gabon yamthibitisha kiongozi wa kijeshi Nguema mshindi rasmi wa uchaguzi wa urais

Brice Oligui Nguema alipata 94.85% ya kura ikilinganishwa na mpinzani wake mkuu, Alain-Claude By-Nze, aliyepata 3.11%, kulingana na matokeo rasmi ya mwisho.
25 Aprili, 2025
Shirika la Umoja wa Mataifa limefikia watu milioni 4 Sudan lakini linaonya kuhusu njaa kali

Mratibu wa shughuli za dharura anasema Sudan ni nchi pekee ambayo imethibitika kuwa na njaa kali, huku watu milioni 25 wakiwa hawana chakula
25 Aprili, 2025
Uchunguzi wa huduma za mauzo ya viungo nchini Kenya waanza

Kamati huru itafanya ukaguzi wa kina wa huduma zote za upandikizaji wa figo katika hospitali ya Mediheal iliyopo kaunti ya Eldoret katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, baada ya hospitali hiyo kushutumiwa kwa kuhusika na mauzo ya figo.
25 Aprili, 2025
Rwanda kuanza kutibu wagonjwa bila kuhudhuria vituo vya afya

Hospitali zitatumia teknolojia maarufu kama ‘telemedicine,’ mbinu inayotumia teknolojia ya kidijitali kama vile simu za video, programu za simu na majukwaa ya mtandaoni kutoa huduma za afya kwa mbali.
25 Aprili, 2025

Raia wa Rwanda afunguliwa mashtaka Marekani kwa kuhusika na mauaji ya kimbari

Dunia yaadhimisha siku ya malaria, nchi 9 Afrika bila malaria

Marekani kuwa mwenyeji wa makubaliano kati ya Rwanda na DRC

Kenya yaamua tena hisabati kuwa somo la lazima

Msumbiji yatangaza kumalizika kwa uasi katika mkoa wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado
25 Aprili, 2025
Rais wa Afrika Kusini Ramaphosa kukutana na Trump ‘karibuni’ kusuluhisha matatizo yao
Viongozi hao wawili watajadili kuhusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili baada ya serikali ya Trump kusitisha misaada ya fedha kwa Afrika Kusini na kumtimua balozi wao.

25 Aprili, 2025
Magaidi wa al-shabaab wavamia kambi ya jeshi Somalia, watu kadhaa wauawa
Kundi lenye ushirikiano na al-Qaeda limedai kuvamia kambi ya Wargaadhi, lakini Wizara ya Ulinzi ya Somalia inakanusha hilo na kusema kuwa bado kambi hiyo iko chini ya udhibiti wa jeshi la taifa

25 Aprili, 2025
Jeshi la Sudan lasema limewaua wapiganaji 60 wa RSF Darfur Kaskazini
Tangu Mei 2024 kumekuwa na mapigano makali El-Fasher kati ya jeshi la Sudan na RSF

24 Aprili, 2025
Rais wa Ukraine kukatisha ziara yake ya Afrika Kusini
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema amelazimika kukatisha sehemu ya ratiba yake nchini Afrika Kusini baada ya shambulizi la Urusi katika mji mkuu wa Kyiv.

24 Aprili, 2025
Rwanda yazindua mikakati mipya ya kuthibiti malaria
Mbinu mpya inahusisha kupima familia yote baada ya mtu mmoja kugundulika kuwa na ugonjwa wa malaria ili kutambua na kutibu wengine ambao wanaweza kuambukizwa lakini bado hawana dalili.

24 Aprili, 2025
Mahakama ya Senegal yazuia ombi la serikali la kufuta sheria ya msamaha kwa ‘wahalifu’
Baraza la Katiba la Senegal lilitangaza sheria mpya ya msamaha kuwa kinyume na katiba, na hivyo kuzua mvutano mpya wa kisiasa kati ya wapinzani.

24 Aprili, 2025
Serikali ya DRC, M23 wakubali kufanya mazungumzo
Taarifa iliyotolewa katika mazungumzo imethibitisha kwamba pande zote mbili zimekubaliana kusitisha mapigano mara moja.

24 Aprili, 2025
Waliojaribu kutorosha siafu kupitia JKIAkuhukumiwa mwezi ujao
Washukiwa hao wanne wamekiri makosa yao wiki iliyopita baada ya mamlaka kuwakamata wakiwa na siafu 5,000.

24 Aprili, 2025
Djibouti yawapa wahamiaji haramu wiki moja kuondoka au wawaondowe kwa lazima
Raia wengi wa kigeni wanapitia nchi hiyo kwa lengo la kuanza safari ya hatari kupitia Bahari ya Shamu kwa kutumia maboti yaliyojaa kupitiliza.

23 Aprili, 2025
Wafugaji wenye silaha wawaua watu 11 katika mashambulizi mengine Nigeria
Kumekuwepo na ongezeko la mapigano katika eneo hilo katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita kati ya wakulima na wafugaji



