25 Aprili, 2025

Dunia yaadhimisha siku ya malaria, nchi 9 Afrika bila malaria

Barani Afrika WHO inasema tangu mwaka wa 2000, zaidi ya wagonjwa wa malaria bilioni 1.7 na vifo milioni 12 vimepukwa katika kanda ya Afrika kutokana na juhudi za kimataifa za afya.

africa usaid malaria 78705

25 Aprili, 2025

Marekani kuwa mwenyeji wa makubaliano kati ya Rwanda na DRC

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio atatia saini ‘tamko la kanuni’, siku chache baada ya kutangazwa kusitishwa kwa mapigano kati ya DRC na waasi wa M23 wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni yaliyofanywa na Qatar huko Doha.

ap25029494435313

25 Aprili, 2025

Kenya yaamua tena hisabati kuwa somo la lazima

Haya yanajiri baada ya Wizara ya Elimu kutangaza kuwa masomo ya hesabu hayatakuwa ya lazima tena kwa wanafunzi wa sekondari chini ya Mtaala unaozingatia Umahiri (CBC), mabadiliko makubwa kutoka kwa mfumo ulioondolewa wa elimu.

education 1

25 Aprili, 2025

Msumbiji yatangaza kumalizika kwa uasi katika mkoa wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado

Jeshi linasema limedhibiti kambi za mwisho za mafunzo ambazo bado zilikuwa zinatumiwa na waasi katika mkoa wa kaskazini mwa nchi wa Cabo Delgado.

cabod 20delgado

25 Aprili, 2025

Rais wa Afrika Kusini Ramaphosa kukutana na Trump ‘karibuni’ kusuluhisha matatizo yao

Viongozi hao wawili watajadili kuhusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili baada ya serikali ya Trump kusitisha misaada ya fedha kwa Afrika Kusini na kumtimua balozi wao.

trump 20rama

25 Aprili, 2025

Magaidi wa al-shabaab wavamia kambi ya jeshi Somalia, watu kadhaa wauawa

Kundi lenye ushirikiano na al-Qaeda limedai kuvamia kambi ya Wargaadhi, lakini Wizara ya Ulinzi ya Somalia inakanusha hilo na kusema kuwa bado kambi hiyo iko chini ya udhibiti wa jeshi la taifa

somalia

25 Aprili, 2025

Jeshi la Sudan lasema limewaua wapiganaji 60 wa RSF Darfur Kaskazini

Tangu Mei 2024 kumekuwa na mapigano makali El-Fasher kati ya jeshi la Sudan na RSF

1745499118161 3qdw45 sudan 20wakimbizi 20

24 Aprili, 2025

Rais wa Ukraine kukatisha ziara yake ya Afrika Kusini

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema amelazimika kukatisha sehemu ya ratiba yake nchini Afrika Kusini baada ya shambulizi la Urusi katika mji mkuu wa Kyiv.

south africa ukraini zelenskyy 75251

24 Aprili, 2025

Rwanda yazindua mikakati mipya ya kuthibiti malaria

Mbinu mpya inahusisha kupima familia yote baada ya mtu mmoja kugundulika kuwa na ugonjwa wa malaria ili kutambua na kutibu wengine ambao wanaweza kuambukizwa lakini bado hawana dalili.

2024 12 11t080201z 2126097288 rc2kr5ayehpp rtrmadp 3 health malaria who

24 Aprili, 2025

Mahakama ya Senegal yazuia ombi la serikali la kufuta sheria ya msamaha kwa ‘wahalifu’

Baraza la Katiba la Senegal lilitangaza sheria mpya ya msamaha kuwa kinyume na katiba, na hivyo kuzua mvutano mpya wa kisiasa kati ya wapinzani.

senegal
Inapakia...