Wanajeshi wamepelekwa katika mitaa ya mji mkubwa zaidi nchini Afrika Kusini siku ya Jumatani baada ya rais kutangaza mwezi uliopita kuwa ataagiza wanajeshi kusaidiana na polisi katika kukabiliana na vurugu za magenge na uchimbaji haramu wa madini.
Nchi hiyo ina kiwango kikubwa cha mauaji karibu watu 60 huuawa kila siku ikiwemo mapigano kati ya magenge ya dawa za kulevya katika maeneo ya mji wa Cape Town na kufyatuliana risasi kunakohusishwa na uchimbaji haramu wa madini katika mji wa mkoa wa Gauteng, Johannesburg.
Chanzo:TRT Afrika














