Maelfu ya raia katika Sudan Kusini wamelazimika kukimbilia Ethiopia baada ya jeshi kuamuru kuondolewa kwa watu katika mji wa Akobo mapema mwezi huu.
Kwa mujibu wa UNICEF, takriban watu 100,000 wamevuka mpaka huku wengine wakihamia maeneo salama ndani ya nchi.
Mapigano makali kati ya serikali na upinzani katika jimbo la Jonglei yameongeza hofu ya kurejea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Ripoti zinaeleza kuwa hospitali ya Akobo imeporwa na kufungwa, huku hali ya watoto waliokimbia makazi yao ikiwa mbaya kutokana na utapiamlo.
CHANZO: TRT Afrika














