Wanamgambo wa Boko Haram wamewaua wanajeshi wasiopungua 12 na raia watatu katika mashambulizi ya usiku yaliyofanyika katika majimbo ya Borno na Yobe kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Mashambulizi hayo yalilenga maeneo ya Kukawa, Dalwa na Goniri, ambapo mapigano kati ya wanamgambo na jeshi yalidumu kwa saa kadhaa. Pia nyumba zaidi ya 250 ziliripotiwa kuchomwa moto.
Jeshi la Nigeria limekuwa likiongeza operesheni dhidi ya makundi ya kigaidi mwaka huu, huku mashambulizi haya yakitokea muda mfupi baada ya onyo la kijasusi kuhusu uwezekano wa shambulio.
CHANZO: TRT Afrika














