Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amezindua rasmi kampuni ya kwanza ya bima ya Kiislamu nchini humo inayojulikana kama Tamini General Insurance. Hatua hiyo inaashiria kuanzishwa kwa mfumo wa bima unaofuata misingi ya Kiislamu ya kusaidiana na kugawana hatari.
Kampuni hiyo itafanya kazi kwa ushirikiano na Salaam Bank, benki ya Kiislamu inayotoa huduma za kifedha bila riba. Mfumo huu unalenga kutoa mikopo kwa misingi ya uzalishaji badala ya matumizi ya kawaida, sambamba na kuhakikisha ushiriki wa wateja katika kugawana faida na hasara.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Rais Museveni alisema mpango huo unaendana na utamaduni wa jadi wa kusaidiana. Alisisitiza umuhimu wa kukopa kwa ajili ya uwekezaji na uzalishaji, na kuongeza kuwa huduma hiyo itawafikia pia watu wa kipato cha chini ili kuwapa fursa zaidi za kifedha.
CHANZO: TRT Afrika














