Afrika

Wanajeshi wa Afrika Kusini wafariki wakikabiliana na wachimba madini haramu

Vifo hivi ni vya kwanza tangu Rais Ramaphosa alipopeleka wanajeshi kukabiliana na uchimbaji madini haramu.

Newstimehub

Newstimehub

18 Julai, 2026

fb6f0ff3 35d5 415b b64d 59fa43b29d54 1780073850932

Wanajeshi wawili wa Afrika Kusini wameanguka katika mgodi wakati wa operesheni ya kukabiliana na uchimbaji madini haramu, msemaji wa polisi amesema.

Vifo hivyo ni vya kwanza kutokea tangu Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kupeleka wanajeshi mwezi Machi kusaidia operesheni ya polisi dhidi ya uchimbaji madini haramu.

Tukio hilo limetokea siku ya Ijumaa katika mgodi uliotelekezwa magharibi mwa Johannesburg ambapo wanajeshi walikuwa wanawafuatilia wachimba migodi haramu, wanaojulikana kama “zama zama,” amesema msemaji wa polisi Athlenda Mathe.

Wanajeshi walianguka katika mgodi uliotelekezwa, amesema.

‘Wanajeshi wenye ujasiri’

Jeshi la Ulinzi la Taifa la Afrika Kusini (SANDF) limesema tukio hilo limetokea saa kumi na mbili alfajiri.

Limesema jitihada zinaendelea za kuwatambua rasmi wanajeshi hao na kuzijulisha familia zao.

“Ni pigo kubwa kwa ulinzi na kwa taifa kwa ujumla kupoteza wanajeshi hawa,” amesema kaimu Waziri wa Polisi Firoz Cachalia.

Wengi wa wachimbaji haramu ni raia kutoka mataifa jirani.