Afrika

Chama cha upinzani Tanzania CHAUMMA, kimezindua rasmi Jumapili Kampeni yake ya Urais

Katika hotuba yake, mgombea Urais Salum Mwalimu alizungumzia uwezeshaji wa watu mashinani, na kupendekeza uingiliaji kati wa moja kwa moja kama kufufua uchumi wa ndani na viwanda vya enzi za ukoloni.

Newstimehub

Newstimehub

31 Agosti, 2025

e06ebff2eb34ec173ff4a1c7506fc15b72cb5dc796f0f848d0ec40fa5be14f8d

Vyama vya upinzani CHAUMMA na CUF Jumapili wamezindua rasmi kampeni zao za urais leo, ikiwa ni ishara ya kuanza rasmi harakati zao kuelekea uchaguzi mkuu wa Tanzania.

Uzinduzi wa kampeni ya leo ulijumuisha taarifa kwa umma kuthibitisha dhamira ya CHAUMMA ya kuongeza furaha miongoni mwa Watanzania, kupunguza ukosefu wa ajira, na kufufua sekta za kiuchumi kama pamba na viwanda.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo katika viwanja vya Biafra, Kinondoni jijini Daresalaam, mgombea wa urais wa chama hicho Salum Mwalimu alisisitiza lengo lake la kutoa elimu bila malipo kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu kwa kufuata maono ya muda mrefu ya mwanzilishi Hashim Rungwe.

‘‘Uchaguzi huu wa 2025, sio uchaguzi wa kawaida, ni uchaguzi wa maamuzi magumu. Ni uchaguzi wa kuamua kuendelea na hisoria ya maumivu, ahadi hewa na umasikini,’’ alisema Mwalimu. ‘‘ Au tunaanza ukurasa mpya wa maendeleo ambao kwa miaka 63 ya uhuru, serikali zote za CCM zimeshindwa kutumia fursa za rasli mali nyingi kuleta maendeleo.’’ aliongezea.

Mkutano huo ulisisitiza uwezeshaji wa watu mashinani, na kupendekeza uingiliaji kati wa moja kwa moja kama kufufua uchumi wa ndani na viwanda vya enzi za ukoloni, kando na maendeleo ya miundombinu ili kukuza ukuaji shirikishi.