Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimefungua kesi katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ), kikipinga uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzima huduma za intaneti kati ya Oktoba 29 na Novemba 4, 2025. Wanaharakati wanadai kuwa hatua hiyo iliathiri haki za msingi za raia na ni kinyume na katiba. Waliopo katika kesi hiyo ni pamoja na Waziri wa Mawasiliano, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mwanasheria Mkuu wa Serikali na baadhi ya makampuni ya simu. Wanataka uamuzi huo uharimishwe, kuzuia hatua kama hizo siku zijazo, na kuanzishwa kwa msahama wa wazi. Wakati huo huo, Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimeishitaki serikali kwa zuio la siku tano la kutotoka nje jijini Dar es Salaam.
CHANZO: TRT Afrika














