Akizungumza na TRT World, Fidan alisema mashambulizi ya kulipizana yameathiri moja kwa moja Uturuki, ikiwemo kulengwa kwa meli za biashara na kuingia kwa ndege zisizo na rubani katika anga yake. Alisisitiza kuwa hatari hiyo inaathiri pia nchi jirani kama Romania na Bulgaria, na akaonya kuwa bila kusitishwa kwa mapigano, mgogoro huo unaweza kuenea zaidi barani Ulaya.
CHANZO: TRT Afrika














