Siasa Uturuki

Hakan Fidan: Ukosefu wa Dhamira ya Kisiasa Ndiyo Unakwamisha Uturuki Kujiunga na EU

Waziri wa Mambo ya Nje asema Ankara imetimiza masharti mengi lakini EU haina nia ya kweli ya kuikubali.

Newstimehub

Newstimehub

29 Aprili, 2026

742

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, amesema kikwazo kikuu kinachozuia nchi yake kujiunga na Umoja wa Ulaya (EU) si masharti wala mageuzi, bali ni ukosefu wa dhamira ya kisiasa kutoka kwa EU.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Austria, Beate Meinl-Reisinger, Fidan alisema Uturuki haijawahi kuomba kupewa upendeleo maalum au kuingizwa bila kutimiza masharti ya uanachama.

Alisema tatizo kubwa ni kwamba hakuna dhamira ya kisiasa ndani ya EU inayosema wazi kuwa Uturuki itakubaliwa mara tu itakapokamilisha vigezo vinavyotakiwa.

Fidan alisisitiza kuwa umuhimu wa kimkakati wa Uturuki umeonekana zaidi katika vita vya Urusi na Ukraine, lakini bado Brussels inaonekana kusita.

CHANZO: TRT Afrika