Rais Nicolas Maduro amesema vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya meli za mafuta za Venezuela ni jaribio la kuigeuza nchi yake kuwa koloni la kigeni na akasisitiza kuwa juhudi zozote za kuipindua serikali yake zitashindwa. Kauli hiyo imekuja kufuatia tangazo la Rais Donald Trump kuhusu hatua za kuzuia meli zilizowekewa vikwazo, akidai Venezuela sasa iko chini ya shinikizo la kijeshi la Marekani. Umoja wa Mataifa na viongozi wa kikanda, akiwemo Rais wa Mexico Claudia Sheinbaum, wametoa wito wa kupunguza mvutano na kurejea kwenye mazungumzo, huku Baraza la Wawakilishi la Marekani likipiga kura kukataa azimio la kuhitaji idhini ya Congress kabla ya hatua za kijeshi dhidi ya Venezuela.
CHANZO: BBC NEWS














