Uturuki Ulimwengu

Uturuki na Iran wazidisha mawasiliano kupunguza mvutano wa kikanda

Mazungumzo ndiyo njia bora ya kupunguza mvutano wa kikanda.

Newstimehub

Newstimehub

15 Januari, 2026

277

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, na wa Iran, Abbas Araghchi, wamefanya mawasiliano mara mbili ndani ya saa 24, wakisisitiza umuhimu wa mazungumzo kama njia ya kupunguza mvutano unaoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati.

Mazungumzo ya simu ya Jumatano yalifuatia mawasiliano ya awali siku ya Jumanne, hatua inayoonyesha juhudi za kidiplomasia za mataifa hayo mawili. Vyanzo vya kidiplomasia vya Uturuki vimesema Fidan alisisitiza kuwa mazungumzo ndiyo njia bora ya kupunguza hali ya wasiwasi wa kikanda.

Iran kwa sasa inakabiliwa na maandamano makubwa yaliyosababishwa na kushuka kwa thamani ya sarafu ya rial na hali mbaya ya uchumi. Serikali ya Tehran imezituhumu Marekani na Israel kwa kuunga mkono kile ilichokiita “ghasia” na “ugaidi.”

Kundi moja la haki za binadamu lenye makao Marekani linakadiria kuwa zaidi ya watu 2,550 wamefariki tangu maandamano kuanza, huku zaidi ya 1,134 wakijeruhiwa, ingawa hakuna takwimu rasmi zilizotolewa na serikali ya Iran.

CHANZO: TRT Afrika