Afrika

Rais wa Côte d’Ivoire Ouattara amteua kaka yake kama makamu wa waziri mkuu

Kakake rais, Tene Birahima Ouattara, atashikilia nafasi hiyo mpya pamoja na wizara ya ulinzi.

Newstimehub

Newstimehub

24 Januari, 2026

9f6fd99397ee4bf8c020722d42edc16b992ec1740ee422d7ac4c2b64608b8ebc

Rais wa Côte d’Ivoire Alassane Ouattara alifanyia mabadiliko baraza lake la mawaziri siku ya Ijumaa, na kudumisha mawaziri wengi huku akimteua kaka yake, Waziri wa Ulinzi, Tene Birahima Ouattara, katika nafasi mpya ya makamu wa waziri mkuu, ambayo ataishikilia pamoja na wizara yake ya ulinzi.

Hatua hiyo inamwinua Ouattara mdogo ndani ya uongozi wa serikali, wakati nyadhifa nyingi muhimu zilibakia bila kubadilika, kuashiria mwendelezo badala ya urekebishaji wa kina.

Mabadiliko hayo yanafuatia kuchaguliwa tena kwa Ouattara mwezi Oktoba na ushindi wa chama chake katika uchaguzi wa wabunge wa Desemba, na kupata wabunge wengi.

Ouattara, 84, naibu mkurugenzi mkuu wa zamani wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, ameiongoza nchi hiyo tangu 2011 na amesema kuwa anakusudia kuandaa mazingira ya kizazi kipya cha viongozi wa kisiasa katika kipindi chake cha uongozi.

Mabadiliko hayo yanakuja wakati Côte d’Ivoire, mzalishaji mkubwa zaidi wa kakao duniani, inataka kuendeleza karibu miaka 15 ya ukuaji endelevu wa uchumi ambao umeifanya kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi zaidi katika eneo hilo.