Serikali ya Msumbiji imezindua mtambo mpya wa kuchakata madini ya grafiti wenye thamani ya takribani dola milioni 150, hatua inayolenga kuongeza thamani ya madini hayo kwa mauzo ya nje. Mtambo huo una uwezo wa kuzalisha hadi tani 200,000 za grafiti kwa mwaka.
Kwa sasa, Msumbiji inaongoza kwa uzalishaji wa grafiti barani Afrika, ikifuatiwa na Madagascar na Tanzania. Hata hivyo, ripoti ya Taasisi ya Jiolojia ya Marekani inaonyesha uzalishaji wa kimataifa ulipungua kutoka tani 98,000 mwaka 2023 hadi tani 75,000 mwaka 2024.
Grafiti imeendelea kuwa na soko kubwa duniani kutokana na mahitaji yake makubwa katika utengenezaji wa bidhaa muhimu, hususan betri za magari ya umeme na matumizi mengine ya viwandani.
CHANZO: TRT Afrika














