Uturuki

Uturuki yapata makubaliano ya awali ya dola bilioni 6.75 kwa mradi mpya wa reli Istanbul

Mradi mpya wa reli utakaovuka Bosphorus unalenga kuunganisha viwanja vikuu vya ndege na kupunguza msongamano wa usafiri jijini Istanbul.

Newstimehub

Newstimehub

25 Februari, 2026

432

Serikali ya Türkiye imefikia makubaliano ya awali ya ufadhili wa dola bilioni 6.75 na taasisi sita za kimataifa kwa ajili ya ujenzi wa reli mpya itakayopita kaskazini mwa Istanbul. Waziri wa Uchukuzi Abdulkadir Uraloğlu alisema mradi huo ni miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya miundombinu inayotarajiwa kufadhiliwa kimataifa nchini humo.

Reli hiyo yenye urefu wa kilomita 125 itaunganisha mtandao wa Marmaray karibu na Gebze, Uwanja wa Ndege wa Sabiha Gökçen, Daraja la Yavuz Sultan Selim, Uwanja wa Ndege wa Istanbul hadi eneo la Halkalı, na hivyo kuunda njia mpya ya usafiri yenye uwezo mkubwa.

Mamlaka zinasema mradi huo utapunguza msongamano kwenye reli ya Marmaray kwa kutenganisha usafiri wa abiria na mizigo, huku ukiunganisha kwa mara ya kwanza viwanja viwili vikubwa vya ndege vya Istanbul kupitia reli. Zabuni ya mradi inatarajiwa kukamilika mwaka huu na ujenzi kuanza muda mfupi baada ya hapo.

CHANZO: TRT Afrika