Afrika Uchumi

Mgogoro wa Mashariki ya Kati Wakwaza Biashara ya Nyama Kenya

Kukatizwa kwa usafirishaji baharini na angani kumeathiri sana biashara.

Newstimehub

Newstimehub

4 Mechi, 2026

454

Wafanyabiashara wa nyama nchini Kenya wamelalamika kukwama kwa zaidi ya tani 200 za nyama kwenye maghala baada ya kuzorota kwa biashara kunakosababishwa na mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa Waweru Kamau, Meneja Uzalishaji katika kampuni ya Juja International Abattoirs, kusitishwa kwa baadhi ya njia za usafirishaji kwa njia ya bahari na anga kumeathiri pakubwa mauzo ya bidhaa hiyo nje ya nchi.

Mashariki ya Kati imekuwa soko muhimu kwa nyama ya Kenya, hasa katika nchi kama Falme za Kiarabu, Saudi Arabia, Oman, Qatar na Kuwait. Kupungua kwa usafirishaji kwenda mataifa hayo kumesababisha hasara kwa wazalishaji na wafanyabiashara wa nyama.

Takwimu zinaonyesha kuwa mauzo ya nyama ya Kenya yalifikia shilingi bilioni 18.7 mwaka 2024 (zaidi ya dola milioni 144), yakionyesha ukuaji wa wastani wa asilimia 39 kwa mwaka. Hata hivyo, hali ya sasa inaibua wasiwasi juu ya mustakabali wa sekta hiyo endapo changamoto za kibiashara hazitapatiwa ufumbuzi wa haraka.

CHANZO: TRT Afrika