Serikali ya Tunisia imetangaza mpango wa kupanua Tunis–Carthage International Airport kwa gharama ya takribani dinari bilioni 3 (karibu dola bilioni 1). Lengo ni kuongeza uwezo wa uwanja huo kutoka abiria milioni 5 hadi takribani milioni 18.5 kwa mwaka ifikapo 2031.
Wizara ya Uchukuzi imesema mradi huo umejumuishwa katika bajeti ya uwekezaji ya mwaka 2026 ya mamlaka ya usafiri wa anga. Serikali pia imeamua kwa sasa kuacha mpango wa kujenga uwanja mpya wa ndege na badala yake kuboresha na kupanua uwanja uliopo.
CHANZO: TRT Afrika














