Afrika Mazingira Usalama

Tanzania: Zoezi la kuhama eneo la hifadhi ya Ngorongoro halijafanikiwa

Serikali ya nchi hiyo imekuwa ikihamisha jamii kwenda maeneo yaliyotengwa, kama vile Handeni mkoani Tanga, ili kupunguza mgongano kati ya binadamu na wanyamapori na kuimarisha uhifadhi.

Newstimehub

Newstimehub

12 Mechi, 2026

cc09ed887f81ce55fff10c2ea783fd81c7d6738ecd9d7797716229e29a74b38a

Kulingana na Iyombe, kufikia sasa, ni kaya 1,678 pekee zilizoondoka ndani ya NCA, kati ya kaya 23,000.Mwenyekiti wa Tume iliyopewa jukumu la kutathmini utekelezaji wa zoezi la uhamaji wa hiari kwa Wakazi wa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (NCA) kwenda Msomera mkoani Tanga na maeneo mengine, Mussa Iyombe, amesema zoezi hilo halijafanikiwa kama ilivyotarajiwa.

“Matokeo ya tathmini yanaonesha kuwa dhamira ya serikali ya kutekeleza zoezi la uhamaji wa hiari ili kuboresha maisha ya wananchi na kulinda ikolojia ya Hifadhi ya Ngorongoro,” alisema Iyombe wakati akikabidhi ripoti ya tume hiyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Machi 12, 2026.

Chanzo: TRT Afrika