Afrika Siasa

Waziri Mkuu wa Libya Afanya Mabadiliko Serikalini

Waziri Mkuu wa Libya, Abdulhamid Dbeibeh, ametangaza mabadiliko katika baraza la mawaziri kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Newstimehub

Newstimehub

12 Mechi, 2026

471

Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid Dbeibeh ametangaza kufanya mabadiliko katika serikali yake akisema hatua hiyo inalenga kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na mtandao wa serikali wa Hakomitna, mabadiliko hayo yamehusisha kubadilishwa kwa mawaziri 10 kati ya mawaziri 27 waliokuwapo.

Hata hivyo, Dbeibeh ataendelea kushikilia nafasi za waziri wa ulinzi pamoja na waziri wa mambo ya nje katika serikali hiyo.

Kiongozi huyo amesema mabadiliko hayo pia yanalenga kupunguza tofauti za kikanda ndani ya serikali na kuhakikisha huduma bora kwa wananchi.

CHANZO: TRT Afrika