“Zaidi ya maafisa wa polisi 1000 kutoka vikundi mbalimbali watapelekwa katika njia za makutano, maeneo ya watazamaji na barabara kuu za kufikia ili kuhakikisha hali ya usalama, pamoja na kudhibiti umati wa watakaojitokeza na kusaidia udhibiti wa msongamano wa magari,” Wizara ya Mambo ya Ndani ilisema katika taarifa yake.

Wizara ya Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa imepiga marufuku utumiaji wa ndege zisizo na rubani katika maeneo yaliyotengwa ndani ya Naivasha na maeneo jirani wakati wa WRC Safari Rally Kenya 2026. Imesema hii ni ehemu ya hatua za usalama kwa watazamaji wa mashindano hayo yanayoingia siku ya pili.
Mashindano ya mwaka huu yatakuwa na changamoto kidogo kwa sababu barabara zimejaa maji na matoke, kutokana na msimu wa mvua unaoendelea.

“Zaidi ya vumbi hili, Safari Rally ni injini ya mabilioni ya shilingi. Inaendesha asilimia 100 ya hoteli za mitaani, umiliki wa hoteli za Nakuru kwa asilimia 100. Pia ni asili ya ajabu kwa zaidi ya watazamaji milioni 80 ulimwenguni,” Miano aliongezea.

“Zaidi ya msisimko ambapo vumbi huinuka na injini kuunguruma – magari yanapita katika mandhari ya kuvutia ya Kenya, kutoka maeneo ya ajabu ya Bonde la Ufa hadi nyanda za Hifadhi ya Kitaifa ya Hell’s Gate, na maji tulivu ya Ziwa Naivasha,” Bodi ya Utalii ya Kenya ilisema katika akaunti yake ya X.
Chanzo: TRT Afrika














