Mahakama ya shirikisho katika jimbo la Massachusetts imesitisha kwa muda uamuzi wa serikali ya Marekani wa kumaliza hadhi ya Temporary Protected Status kwa wahamiaji kutoka Somalia.
Jaji Allison D. Burroughs amesema hatua hiyo inaweza kuwa na athari kubwa ikiwa itatekelezwa haraka.
Uamuzi huo unamaanisha kuwa Wasomali walio na TPS wataendelea kuwa na haki ya kufanya kazi na kulindwa dhidi ya kufukuzwa nchini kwa sasa.
CHANZO: TRT Afrika













