Nchi ya Chad imetajwa kuwa na kiwango kikubwa zaidi cha uchafuzi wa hewa barani Afrika mwaka 2025, kulingana na ripoti ya shirika la ufuatiliaji wa ubora wa hewa la IQAir. Ripoti hiyo imeonyesha kuwa viwango vya chembechembe hatari za PM2.5 vimepita kiwango kilichopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Uchafuzi huo unahatarisha afya ya wananchi, hasa watoto na wazee. Wataalamu wanasema hali hiyo inachangiwa kwa kiasi kikubwa na vumbi kutoka maeneo ya kaskazini ya nchi hiyo pamoja na hali ya hewa yenye upepo mkali.
CHANZO: TRT Afrika














