Ripoti mpya ya “State of African Governance: Forces of the Future” imeonesha picha mchanganyiko kuhusu hali ya kisiasa barani Afrika, ikibainisha mafanikio fulani pamoja na changamoto zinazoendelea.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, masuala ya utawala bora, uhalali wa viongozi, ushirikiano wa kimataifa na ushawishi wa kisiasa yatachukua nafasi kubwa katika kuunda mwelekeo wa kisiasa wa Afrika mwaka 2026.
Ingawa kuna dalili za maendeleo katika baadhi ya nchi, ripoti inaonya kuwa bado kuna matatizo katika mifumo ya uchaguzi. Wataalamu wanasema kuwa hata pale uchaguzi unapofanyika kwa amani siku ya kupiga kura, mchakato mzima unaweza kuwa na mapungufu yanayoathiri haki na uwazi.
Zaidi ya chaguzi 15 zinatarajiwa kufanyika barani Afrika mwaka huu, jambo linalochukuliwa kama mtihani mkubwa kwa uwezo wa nchi kuhakikisha uchaguzi huru, wa haki na unaoaminika
Chanzo: Africanews














