Wafanyabiashara katika Soko la Gikomba jijini Nairobi wanakabiliwa na hasara kubwa kufuatia ubomoaji uliofanyika usiku kucha. Tingatinga zilibomoa vibanda vingi, hasa katika eneo la viatu, na kuharibu bidhaa za wafanyabiashara wengi.
Tukio hilo limewaacha maelfu bila chanzo cha mapato, huku likizua malalamiko kutokana na madai ya kupuuzwa kwa maagizo ya mahakama yaliyokuwa yamesitisha ufurushaji.
CHANZO: TRT Afrika














