Wafanyabiashara katika Soko la Gikomba wanakabiliwa na hasara kubwa kufuatia ubomoaji wa usiku kucha uliofanywa na mamlaka, katika juhudi za kurejesha ardhi ya kando ya Mto Nairobi.
Mashuhuda wanasema tingatinga zilivamia eneo hilo kuanzia usiku wa manane hadi asubuhi, zikibomoa vibanda vingi hasa katika sehemu ya kuuzia viatu. Bidhaa nyingi ziliharibiwa huku wafanyabiashara wakibaki bila njia ya kujipatia kipato.
Operesheni hiyo ilifanyika baada ya muda wa notisi ya kuondoka kuisha, lakini wafanyabiashara wanadai haikuwa ya haki kwani baadhi yao hawakuwa wamepata muda wa kutosha kujiandaa.
Hatua hiyo imeacha maelfu ya watu bila ajira na kuongeza wasiwasi juu ya mustakabali wa biashara ndogo ndogo katika eneo hilo.
CHANZO: TRT Afrika














