Uturuki imelaani vikali sheria mpya ya hukumu ya kifo iliyoidhinishwa na Knesset, ambayo inadaiwa kulenga mahsusi Wapalestina.
Kupitia Wizara ya Mambo ya Nje, Uturuki imesema sheria hiyo inalenga kuimarisha kile ilichokiita mfumo wa kibaguzi wa Israel dhidi ya Wapalestina.
Taarifa hiyo ilisisitiza kuwa sheria hiyo ni kinyume cha sheria za kimataifa na haina uhalali wowote, huku ikiongeza kuwa ni sehemu ya sera zinazoendelea za ukandamizaji dhidi ya watu wa Palestina.
CHANZO: TRT Afrika














