Mamia ya wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini Afrika Kusini Julius Malema wamejitokeza katika mji wa KuGumpo wakiwa wamevalia mavazi ya rangi nyekundu, wakisubiri hukumu inayotarajiwa dhidi ya kiongozi wao.
Polisi waliimarisha ulinzi mkubwa eneo la mahakama huku wanachama wa chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) wakikusanyika kwa amani kusikiliza hatua za mwisho za kesi hiyo.
Kiongozi mmoja wa EFF alisema: “Hatuko hapa kwa hofu, tuko hapa kumtetea kiongozi wetu.”
Serikali inataka Malema ahukumiwe kifungo cha hadi miaka 15 jela baada ya kupatikana na hatia ya kufyatua risasi hewani mwaka 2018 wakati wa mkutano wa chama hicho.
CHANZO: TRT Afrika














