Michezo

Chelsea Yamfuta Kazi Kocha Liam Rosenior Baada ya Matokeo Mabaya

Klabu yachukua hatua baada ya kupoteza mechi tano mfululizo bila kufunga bao.

Newstimehub

Newstimehub

23 Aprili, 2026

657

Klabu ya Chelsea FC imemtimua kocha wake Liam Rosenior kufuatia matokeo mabaya katika Ligi Kuu ya England.

Rosenior, mwenye umri wa miaka 41, alikuwa ameiongoza timu hiyo kwa zaidi ya miezi mitatu baada ya kujiunga kutoka Strasbourg. Kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya Brighton & Hove Albion kilikuwa mwisho wa safari yake.

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Chelsea kupoteza mechi tano mfululizo za ligi bila kufunga tangu mwaka 1912, hali iliyoweka timu hiyo katika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi.

Klabu ilisema kuwa matokeo na kiwango cha uchezaji “kimeshuka chini ya viwango vinavyotarajiwa,” na kuongeza kuwa Calum McFarlane atachukua nafasi ya kocha wa muda.

CHANZO: TRT Afrika