Tume ya uchunguzi iliyoundwa na serikali ya Tanzania imethibitisha kuwa watu wasiopungua 518 walipoteza maisha wakati wa vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Ripoti hiyo iliwasilishwa chini ya uongozi wa Mohamed Chande Othman, ambaye alisema idadi hiyo bado si ya mwisho.
Rais Samia Suluhu Hassan alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa Oktoba 29 kwa asilimia 98 ya kura, lakini matokeo hayo yalifuatiwa na maandamano katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Tume hiyo pia ilisema madai ya kuwepo kwa makaburi ya halaiki hayakuweza kuthibitishwa, huku ikiongeza kuwa baadhi ya picha zilizosambaa mtandaoni zilikuwa zimehaririwa kwa kutumia akili mnemba.
CHANZO: TRT Afrika














