Uchumi Ulimwengu

Pentagon Yaonya: Uondoaji wa Mabomu Hormuz Waweza Kuchukua Miezi Sita

Ripoti ya Pentagon yaashiria athari za muda mrefu kwa uchumi wa dunia.

Newstimehub

Newstimehub

23 Aprili, 2026

667

Pentagon imewaeleza wabunge wa Marekani kuwa inaweza kuchukua hadi miezi sita kuondoa mabomu ya baharini katika Mlango Bahari wa Hormuz.

Kwa mujibu wa ripoti ya The Washington Post, tathmini hiyo iliwasilishwa kwa Kamati ya Huduma za Kijeshi ya bunge, ikionyesha kuwa hali hiyo inaweza kuathiri uchumi wa dunia kwa muda mrefu.

Maafisa walisema kuwa hali hii inaweza kusababisha bei ya mafuta kuendelea kuwa juu hata baada ya makubaliano yoyote ya amani kati ya Marekani na Iran.

Inadaiwa kuwa Iran inaweza kuwa imeweka zaidi ya mabomu 20 kwa kutumia teknolojia ya GPS, jambo linalofanya kazi ya kuyaondoa kuwa ngumu zaidi.

CHANZO: TRT Afrika