Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuwa watu wanaolalamikia gharama kubwa ya mafuta lakini hawana uwezo wa kuyagharamia wanapaswa kubaki majumbani.
Akizungumza jijini Nairobi katika Mkutano wa “Africa We Build 2026”, Museveni alitoa kauli hiyo kali wakati akijibu maswali kuhusu ongezeko la bei ya mafuta katika Afrika Mashariki.
Alisisitiza kuwa suala muhimu zaidi si mafuta ya magari binafsi, bali mafuta ya ndege (kerosene), ambayo alisema yana mchango mkubwa katika sekta ya utalii na usafirishaji wa mizigo.
Museveni aliongeza kuwa serikali zinapaswa kuweka kipaumbele katika kupunguza bei ya mafuta ya ndege kuliko kushughulikia malalamiko ya waendesha magari na pikipiki.














