Uturuki imelaani vikali mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea katika maeneo mbalimbali ya Mali, ikiyataja kuwa ya kinyama na ya kusikitisha.
Milipuko mikubwa na mashambulizi ya risasi yaliripotiwa Jumamosi katika mji mkuu Bamako, pamoja na Gao, Kidal na mji wa Sévaré.
Katika taarifa rasmi, Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki ilisema inaungana na wananchi wa Mali katika kipindi hiki kigumu na kuahidi kuendelea kuisaidia nchi hiyo katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Jeshi la Mali lilisema hali ipo chini ya udhibiti na kwamba makundi ya kigaidi yaliyoshambulia maeneo kadhaa, yakiwemo kambi za kijeshi, yamepata hasara kubwa.
Uturuki pia ilituma salamu za rambirambi kwa familia za waliopoteza maisha pamoja na wananchi wa Mali.
CHANZO: TRT Afrika

















