Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye ameteuliwa rasmi na chama tawala cha CNDD-FDD kuwa mgombea wake katika uchaguzi wa urais utakaofanyika mwaka ujao.
Katika taarifa iliyotolewa na chama hicho, Ndayishimiye ametajwa kuwa chaguo rasmi la kuwania muhula mpya wa miaka saba.
Ndayishimiye, mwenye umri wa miaka 57, amekuwa rais wa Burundi tangu mwaka 2020 baada ya kurithi madaraka kufuatia kifo cha rais wa zamani Pierre Nkurunziza.
Hadi sasa, tarehe rasmi ya uchaguzi huo haijatangazwa.














