Iran imependekeza kufunguliwa tena kwa Mlango wa Hormuz pamoja na kusitishwa kwa vita, huku mazungumzo kuhusu mpango wake wa nyuklia yakiahirishwa hadi baadaye, kwa mujibu wa ripoti ya vyombo vya habari.
Pendekezo hilo limeripotiwa kuwasilishwa kwa Marekani kupitia wapatanishi akiwemo Pakistan, wakati mvutano wa kidiplomasia ukiendelea kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.
Kwa mujibu wa mpango huo, kusitishwa kwa mapigano kutarefushwa kwa muda mrefu au kufanywa kuwa kwa kudumu, huku mazungumzo ya nyuklia yakianza baada ya Mlango wa Hormuz kufunguliwa tena na vizuizi vya usafiri kuondolewa.
CHANZO: TRT Afrika














