Rais wa Tunisia Kais Saied amemfuta kazi Waziri wa Nishati Fatma Thabet siku ya Jumanne, katika kipindi ambacho nchi hiyo inakabiliwa na mjadala mkali kuhusu miradi ya nishati mbadala.
Kwa mujibu wa taarifa za serikali, Rais Saied amemteua Waziri wa Makazi na Miundombinu Salah Eddine Zouari kwa muda kusimamia wizara hiyo bila kutoa maelezo ya kina kuhusu uamuzi huo.
Mabadiliko hayo yanakuja wakati serikali ikijiandaa kuwasilisha bungeni mswada wa miradi ya nishati mbadala yenye uwezo wa kuzalisha megawati 600 na uwekezaji wa takribani euro milioni 500 (dola milioni 585).
CHANZO: TRT Afrika
















