Wanawake wa Afghanistan wamepata matumaini mapya baada ya kuruhusiwa kurejea kwenye mashindano ya kimataifa ya mpira wa miguu.
Shirikisho la soka duniani, FIFA, limefanya mabadiliko ya kanuni zake ili kuruhusu wachezaji wa kike wa Afghanistan walioko uhamishoni kushiriki mashindano rasmi ya kimataifa.
Hatua hiyo inakuja baada ya wanawake kuzuiwa kushiriki michezo tangu mwaka 2021, wakati utawala wa Taliban uliporejea madarakani na kuweka vikwazo vikali dhidi ya wanawake.
Sasa timu mpya inayojulikana kama Afghan Women United, inayoundwa na wachezaji waliokimbia nchi, inatarajiwa kushiriki mechi za kimataifa kuanzia mwezi Juni.
Wadau wa michezo na haki za binadamu wanasema uamuzi huo ni muhimu kwa sababu unatoa nafasi kwa wanawake kuonyesha vipaji vyao na pia kuwakilisha sauti ya wanawake wa Afghanistan duniani.
Chanzo:BBC














