Rais wa Urusi Vladimir Putin amependekeza usitishaji wa vita wa muda nchini Ukraine wakati wa maadhimisho ya Victory Day ya Mei 9, kulingana na Kremlin.
Pendekezo hilo lilitolewa katika mazungumzo ya simu kati ya Putin na Rais wa Marekani Donald Trump yaliyodumu karibu saa moja.
Kwa mujibu wa mshauri wa Kremlin Yury Ushakov, Putin alimjulisha Trump kuwa Urusi iko tayari kutangaza mapatano ya muda ya kusitisha mapigano wakati wa sherehe za kuadhimisha ushindi wa Umoja wa Kisovieti dhidi ya Ujerumani ya Nazi katika Vita vya Pili vya Dunia.
Trump ameripotiwa kuunga mkono wazo hilo, hatua inayoonekana kama ishara nadra ya makubaliano kati ya Washington na Moscow kuhusu mzozo wa Ukraine.
CHANZO: TRT Afrika














