Kiongozi Mkuu wa Iran, Mojtaba Khamenei, amesema kuwa hali mpya ya kisiasa na kijeshi inaanza kujitokeza katika Ghuba ya Uajemi na Mlango wa Hormuz kufuatia kile alichokiita kushindwa kwa Marekani katika mipango yake dhidi ya Iran.
Katika ujumbe uliorushwa kupitia televisheni ya serikali, Khamenei alisema miezi miwili baada ya Marekani kuongeza uwepo wake wa kijeshi katika eneo hilo, mazingira yanaanza kubadilika kwa namna mpya inayobeba athari za kimkakati katika Mashariki ya Kati.
Kauli hiyo imekuja wakati mvutano kati ya Tehran na Washington ukiendelea kuongezeka kuhusu usalama wa eneo hilo muhimu kwa usafirishaji wa mafuta duniani.
CHANZO: TRT Afrika
















