Afrika

Mlipuko wa Ebola huenda ukawa mbaya zaidi kuwahi kutokea, Afrika CDC yaonya

Kituo cha Afya cha Umoja wa Afrika kinasema kuwa kwa sasa makumi ya maelfu ya watu walioambukizwa ugonjwa huo hawajulikani waliko

Newstimehub

Newstimehub

17 Juni, 2026

772bd493ff0ab4630998ac1517dde5e05dccd0858aee33562db74318df29963e

Mkuu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa barani Afrika, Afrika CDC, ameonya kwamba mlipuko wa Ebola nchini Congo unaweza kuwa mbaya zaidi kuwahi kutokea, akisema kwamba kwa sasa makumi ya maelfu ya watu walioambukizwa ugonjwa huo hawajapatikana.

“Kama hatutakomesha mlipuko huo hivi karibuni utakuwa mbaya zaidi kuliko ilivyokuwa Afrika Magharibi na mashariki mwa DRC,” Mkurugenzi Mkuu wa Afrika CDC Jean Kaseya Jumanne aliambia mkutano wa kawaida wa wakuu wa nchi za Afrika nchini Burundi.

Alikuwa akizungumzia mlipuko ulioathiri Guinea, Liberia na Sierra Leone mwaka 2014-2016 ambao uliua zaidi ya watu 11,000 na mlipuko mbaya sana wa 2018 nchini Congo.

Shirika la Afya Duniani limetangaza dharura ya kiafya ya kimataifa kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambao umesababisha maambukizi 635 yaliyothibitishwa, ikiwa ni pamoja na vifo 127, tangu kutangazwa Mei 15.

Afrika CDC inasema kila mamabukizi iliyothibitishwa inapaswa kusababisha kutambuliwa kwa angalau watu 40.

Hatari kubwa

DRC imefuatilia watu wasiopungua 5,000 wanaohusishwa na maambukizi hayo , wakati idadi inapaswa kuwa karibu 24,000, Kaseya alisema, akiongeza: “Ikiwa hatutafuatilia, inamaanisha kuna hatari kubwa ya maambukizi.”

Kitovu cha mlipuko huo kiko katika jimbo la mashariki la DRC la Ituri, ambako barabara mbovu na ukosefu wa usalama unaochochewa na makundi yenye silaha unatatiza kwa kiasi kikubwa ufikiaji.

Hakuna chanjo au matibabu maalum ya aina ya virusi ya Bundibugyo, ambayo ni nyuma ya mlipuko wa sasa.

Kaseya amehimiza kusitishwa kwa mapigano mashariki mwa DRC ili kuzuia kuenea zaidi, akibainisha: “Mlipuko huu haujui ni nani ni muasi, nani si muasi.”

Ebola huambukizwa kwa njia ya mgusano wa karibu na maji maji ya mwili, na imeua zaidi ya watu 15,000 barani Afrika katika kipindi cha miaka 50 iliyopita.