Afrika Kusini imependekeza kufanya mageuzi makubwa katika sheria zake za muda mrefu zinazodhibiti mtiririko wa fedha, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuifanya nchi hiyo kuwa kitovu kikuu cha kifedha barani Afrika.
Mapendekezo ya Wizara ya Fedha yanajumuisha kuongeza kiwango cha fedha ambazo raia wanaweza kuwekeza nje ya nchi kwa hiari, kudhibiti mali za kidijitali kama cryptocurrency, pamoja na kupunguza vizuizi vya mtiririko wa mitaji.
Serikali inaamini hatua hiyo itasaidia kuvutia uwekezaji mkubwa na kuifanya Afrika Kusini kuwa soko lenye ushindani zaidi kwa wawekezaji wa kimataifa.
CHANZO: TRT Afrika














