Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Waziri Mkuu mteule wa Iraq , Ali Falih Kadhim al-Zaidi, akimpongeza kwa kuteuliwa kuunda serikali mpya ya nchi hiyo.
Katika mazungumzo hayo, Erdogan alieleza imani yake kuwa al-Zaidi ataunda kwa haraka serikali jumuishi, yenye uwiano na utulivu.
Rais huyo wa Uturuki pia alisema Ankara inalenga kuimarisha zaidi ushirikiano wake wa kimkakati na Iraq katika kipindi kipya cha uongozi wa Baghdad.
CHANZO: TRT Afrika














