Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA) limetangaza kuwa litapitia upya mfumo wake wa uuzaji tiketi kuelekea Kombe la Dunia la 2030, kufuatia malalamiko makubwa kuhusu kupanda kwa bei katika mashindano ya 2026 yatakayofanyika Marekani, Mexico na Kanada.
Katibu Mkuu wa FIFA amesema taasisi hiyo inasikiliza maoni ya mashabiki na itafanya tathmini ya jinsi ya kuboresha mfumo wa tiketi kwa mashindano yajayo, ingawa alisisitiza kuwa bei za sasa zinaakisi hali halisi ya soko la Amerika Kaskazini.
CHANZO: TRT Afrika














