Wafanyabiashara wa mafuta nchini Kenya wameanza kuripoti uhaba wa bidhaa hiyo kufuatia athari za vita ya Iran, huku takriban asilimia 20 ya vituo vya mafuta vikidaiwa kuathirika. Mwenyekiti wa Chama cha Vituo vya Mafuta Kenya (POAK), Martin Chomba, amesema hali inaweza kuwa mbaya zaidi ndani ya wiki mbili zijazo.
Ameeleza kuwa kuongezeka kwa gharama za mafuta duniani huku bei za ndani zikibaki bila kubadilika kumeanza kuathiri biashara, na baadhi ya wauzaji wanaweza kuanza kuficha mafuta wakisubiri bei ipande.
CHANZO: TRT Afrika














