Mahakama Kuu nchini Kenya imeidhinisha umri wa lazima wa kustaafu kwa wafanyakazi katika sekta ya umma na kibinafsi, ikitupilia mbali ombi lililotaka kutangaza sera hiyo kuwa kinyume na katiba.
Wafanyakazi wa sekta ya umma na binafsi kupitia sheria ya kustaafu ni kati ya umri wa miaka 60, au 65 kwa watu wenye ulemavu, Mahakama Kuu imesisitiza.
Jaji Lawrence Mugambi alitoa uamuzi huo katika kesi iliyowasilishwa na Charles Chege Gitau, ambaye alidai kuwa kuwataka wafanyakazi kustaafu wakiwa na miaka 60 – au 65 kwa watu wenye ulemavu – ni kulikiuka haki za kikatiba za usawa, utu na mazoea ya haki ya kazi.
“Madai kwamba umri wa lazima wa kustaafu … unabagua kwa sababu unawafanya watu katika jamii hiyo kukosa kazi sio sahihi kabisa, ikizingatiwa kuwa sheria na kanuni zinaruhusu mwajiriwa kubakishwa kwa mujibu wa kandarasi,” Jaji Mugambi alisema.














