Afrika

Urusi na Ethiopia zasaini mpango wa kuanzisha mradi wa nishati ya nyuklia

Urusi na Ethiopia zimesaini mpango wa kuanzisha mradi wa ujenzi wa kiwanda cha nishati ya nyuklia katika nchi hiyo ya Afrika, shirika la habari la TASS limeripoti.

Newstimehub

Newstimehub

26 Septemba, 2025

011bfd7c661cf76adc42a376b22567845cc04a9dd55aa25f17108fb3b4e141eb

Urusi na Ethiopia, zilisaini mpango wa kuanzisha mradi wa kiwanda cha nishati siku ya Alhamisi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Rosatom, Alexey Likhachev, na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia, Gedion Timotheos, walibadilishana hati hiyo jijini Moscow mbele ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin, na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed.

Pande zote mbili pia zilisisitiza ushirikiano katika sekta za nishati na miundombinu.

Rosatom ni shirika la serikali la Urusi linalohusika na nishati ya atomiki, lililoanzishwa mwaka 2007.

Ethiopia na Urusi zilisaini makubaliano ya kiserikali kuhusu ushirikiano katika matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia mwaka 2017, ambayo yaliweka msingi wa ushirikiano mpana zaidi katika sayansi ya nyuklia, teknolojia na elimu.