Tume hiyo ya IEBC ilieleza kuwa itaanza mchakato wa usajili Septemba 29, huku maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2027 yakipamba moto.
Katika taarifa iliyotolewa siku ya Alhamisi, Tume imesema inalenga kupata wapiga kura wapya waliotimiza umri wa miaka 18, na raia wa Kenya ambao hawakuwa wamejisajili awali, pamoja na wale wanaotaka kuhamisha vituo vya kupiga kura.














