Watu wasiopungua 20 wameuawa katika mji wa Mathiang, jimbo la Upper Nile lililopo kaskazini mashariki mwa Sudan Kusini, baada ya mapigano makali kuibuka kati ya vikosi vya serikali, wapiganaji wa upinzani, na makundi yenye silaha, vyombo vya habari vya eneo hilo viliripoti siku ya Jumanne, vikitaja vyanzo vya kijeshi.
Mapigano yalizuka mapema Jumatatu huko Mathiang wakati wapiganaji wa Sudan People’s Liberation Movement-in-Opposition (SPLA-IO) na wale wa White Army waliposhambulia maeneo ya wanajeshi wa Sudan Kusini (SSPDF), afisa mmoja mwandamizi wa jeshi amekiambia kituo cha redio cha Tamazuj siku ya Jumanne.
Mapigano yaliendelea kwa karibu saa tatu na kusababisha mauaji ya wanajeshi wanne wa SSPDF na wapiganaji 16 wa SPLA-IO, Meja Jenerali Khor Chuol Giet alikiambia kituo hicho.
“Tumekuta miili yao 16 katika mahandaki, lakini huenda kukawa na miili zaidi,” aliongeza.
Hali tete














